1.14.2017

KANUNI ZA KUONGEZA FAIDA KATIKA UFUGAJI WA KUKU

Ufugaji kuku ni biashara kama biashara nyingine, kuna wafugaji wengi wanaingia gharama zisizo za lazima katika kufuga kuku hali ambayo inawapelekea kupunguza faida yao na maranyingine hata kutopata faida kabisa, hali hii inawakwaza wafugaji na wengine hukata tamaa kabisa ya kufuga. Lakini hayo yanasababishwa na wao wenyewe wafugaji bila wenyewe kujijua.
Kupitia somo hili tutakumbushana ni namna gani mfugaji anaweza kuzikwepa gharama zisizo za lazima katika ufugaji ili aweze kupata faida mara dufu.

Zifuatazo ni kanuni za kuongeza faida katika ufugaji kuku:-

1. KUPATA VIFARANGA BORA
Vifaranga bora ni wale waliototolewa katiaka wakati uliopendekezwa kitaalaam hali ambayo inamjenga kifaranga kuwa na kinga asilia ya mwili ya kutosha, kwahiyo mfugaji anaweza kufuga hadi kufikia kuuza bila kutumia dawa za kutibu ugonjwa wowote zaidi ya chanjo na dawa za kuanzishia tu, hivyo ataokoa pesa nyingi za kumuita daktari na kununua madawa na faida itaongezeka siku hadi siku. 

2. ULEAJI MZURI (PROPER MANAGEMENT)
Hapa tunakusudia uasafi wa banda, vyombo vya chakula na maji, maji ya kunywa na muhudumu mwenyewe. Kwan magonjwa mengi ya kuku yanasababishwa na uchafu, hivyo uleaji ukiwa mzuri magonjwa hayatakuwepo halikadhalika na na gharama za matibabu hazitakuwepo pia. 

3. CHAKULA BORA
Mfugaji anatakiwa ahakikishe anapata chakula bora kwa ajili ya kuku wake, chakula bora ni ambacho kimekingwa na magonjwa yote na kinakuza kuku kwa wakati, lakin pia chakula bora ni kile ambaho hakisababishi mazingira hatarishi katika banda kama vile kulowesha banda. Chakula ambacho kinalowesha banda kina hatari ya kusababisha magonjwa mbalimbali kama vile coccidiosis na typhoid, hali ambayo mfugaji ataingia gharama za kutibu mara kwa mara na kununua maranda. 

4. KUPATA SOKO LA UHAKIKA
Ili upate soko la uhakika ni lazima uwe na tabia ya kutafuta taarifa (search information), kwa kutafuta taarifa itakuwezesha kujua hali ya soko iliyopo ili nawe uweze kujipanga. Na kama ukiwa unategemea tu mtu wa tenga aje mara nyingi utakuwa unalalamikia soko, hali ambayo itakupa stress na kuuza kuku wako kwa bei ya hasara. Ila kama unajua hali halisi ya soko basi hata akija mtu wa tenga nyumbani hatokudanganya na utakuwa na uhakika na bei yako.

FAIDA ZA UFUGAJI KUKU
Tunafaham kuwa unajua faida za kuku lakini ngoja tukumbushe yafuatayo kuhusu faida za ufugaji kuku.
  • Kuku ni chanzo cha haraka cha pesa kwa kuuza kuku au mayai. 
  • Kuku wanaweza kabisa kukuongezea kipato na kukuondolea kabisa umaskini. 
  • Nyama ya kuku na mayai ni protini muhimu kwa familia, yaan watoto, wagonjwa na hata wazee. 
  • Kinyesi cha kuku pia ni mbolea, lakini kama haitoshi maganda ya mayai na manyoya ni mapambo. 
  • Hakuna dini wala utamaduni wowote Tanzania unaozuia kula kuku. 
  • Katika nyama ambayo haina madhara yoyote katika mwili wa binadamu ni nyama ya kuku na samaki. 
  • Ni mradi unaompa fursa kusimamia hata mwajiriwa bila kuathiri ajira yake. 
  • Na kwa wale akina fulani katika shughuli za kijadi kuku ni moja ya zawadi au malipo kama mteja hana pesa.
Kwa mawasiliano na ushauri piga simu namba:- +255715616331

No comments:

Post a Comment